MICHEZO YOTE

michezo

michezo
simba

Jumanne, 30 Juni 2015

Chile yafuzu fainali za Copa America



Mashabiki wa timu ya ChileMashabiki wa Chile kusubiri Fainali baada ya timu yao kushinda Peru kwenye nusu Fainali
Wenyeji wa kombe la Copa America Chile wamefuzu kufika fainali mara ya kwanza kwa miaka 28. Hii ni baada ya kuwanyuka Peru mabao mawili kwa moja katika mchuano uliofanyika mjini Santiago.
Nusura kiungo wa kati wa Chile Arturo Vidal kuondolewa mapema, hata hivyo bahati mbaya ilikua wa mlinda lango wa Peru Carlos Zambrano aliyepewa kadi nyekundu.
Aliyekua mshambuliaji wa klabu wa QPR ya Uingereza Eduardo Vargas alisaidia Chile kupata bao la kwanza dakika ya 42.
nullEduardo Vargas alisaidia timu yake kupata magoli mawili
Hata hivyo Peru ilisawazisha pale Gary Medel alipojifunga bao. Vargas ndiye aliipatia Chile bao la pili na la ushindi katika dakika ya 64.
Chile haijawahi kushinda kombe la Copa kwa karibu karne moja. Chile wanaingia fainali hapo Jumamosi ambapo huenda wakachuana na Argentina au Paraguay.
Imechapishwa na Unknown kwa 06:00 Hakuna maoni:
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest
Machapisho Mapya Nyumbani
Jisajili kwenye: Machapisho (Atom)

Kunihusu

Unknown
Tazama wasifu wangu kamili

Kumbukumbu la Blogu

  • ▼  2015 (22)
    • ►  Agosti (1)
    • ►  Julai (20)
    • ▼  Juni (1)
      • Chile yafuzu fainali za Copa America
Mandhari ya Alama maalum. Inaendeshwa na Blogger.