michezo

michezo
simba

Jumatano, 1 Julai 2015

HABARI KIMATAIFA

Murray kucheza raundi ya pili Wimbledon

Andy Murray anaungana na Waingereza wenzake watatu kucheza hatua ya pili ya michuano ya tenis ya Wimbledon inayoendelea jijini London, baada ya kumcharaza Mikhail Kukushkin wa Kazakhstan.
Murray, wa tatu kwa ubora duniani alishinda kwa seti 6-4 7-6 (7-3) 6-4 katika mchezo uliodumu kwa saa mbili na dakika 13 wakati hali ya hewa ikiwa nyuzi joto 41 za Selisyasi.
Murray anasema ilikuwa mechi ngumu. Na yeye ndiye aliyeifanya iwe hivyo katika seti ya pili ya mchezo.
Kuingia raundi ya pili Murray anaungana na Waingereza wenzake Liam Broady, Aljaz Bedene na James Ward kutinga raundi ya pili, akiwemo pia Heather Watson namba moja kwa ubora nchini Uingereza kwa upande wa wanawake akimbwaga Caroline Garcia wa Ufaransa kwa seti 1-6 6-3 8-6 .
Hii ni mara ya kwanza kwa Waingereza wanne kwa pamoja kutinga raundi ya pili tangu mwaka 2006. Katika raundi hiyo Murray atakabiliana na Mholanzi Robin Haase, ambaye alimbandua Alejandro Falla wa Colombia kwa seti nne.

amos kunyakuliwa na Machester United?

  • 30 Juni 2015
Sergio Ramos
Timu ya Manchester United ya Uingereza inaamini kuwa Sergio Ramos mwenye umri wa miaka 29 anataka kuondoka Real Madrid baada ya timu hiyo kushindwa kumwongezea mkataba, ambapo mkataba wa sasa unamalizika mwaka 2017.
Manchester United imependekeza kitita cha pauni milioni 28.6 kwa Real Madrid ili kumnyakua mlinzi wake Sergio Ramos.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania ameichezea timu ya Real mara 445.
Ramos alijiunga na Real akitokea timu ya Sevilla mwaka 2005.
Kocha wa Manchester United Louis van Gaal anataka kuimarisha sehemu ya ulinzi ili kuisaidia timu yake kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu ya England ambapo msimu uliopita alishika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo.
Ramos alijiunga na Real akitokea timu ya Sevilla mwaka 2005.
Ameichezea timu ya taifa ya Hispania mara 128 na alikuwa katika kikosi cha kwanza wakati waliposhinda kombe la Ulaya mwaka 2008, 2012 na Kombe la Dunia mwaka 2010.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni