michezo

michezo
simba

Ijumaa, 17 Julai 2015

Tegete 3
PICHA MBALIMBALI ZA TEGETE UWANJANI NDONDO CUP
Ndondo 12


 MAKOCHA YANGA NA GORI MAHIA WAZUNGUMZIA MCHEZO WA KESHO KOMBE LA KAGAME HAPATOSHI UWANJA WA TAIFA JIJINI DARE ESALAAM




KOCHA MKUU WA YA YANGA NA GORI MAHIA PICHANIKocha wa Yanga SC Hans van der Pluijm (kulia) akiwa na kocha wa Gor Mahia Frank Nuttal (kulia)
Makocha wa timu za Yanga na Gor Mahia ya Kenya wamezungumzia mchezo wao wa kesho ambao ndio utakuwa mchezo wa ufunguzi kwenye michuano ya Kagame Cup mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam kuanzia majira ya saa 10:00 za jioni kwa saa za Afrika ya Mashariki.
Kila kocha ametamba kuibulka na ushindi kwenye mchezo huo unaotarajiwa kuwa ni mkali kutokana na ubora wa vikosi vya timu zao. Yanga ndio mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara ambayo ilimalizika mwezi Mei mwaka huu wakati wapinzani wao wakiwa wanaongoza ligi ya Kenya inayoendelea kutimua vumbi nchini humo.
Van Pluijm 1Kocha wa mkuu wa Yanga Hans Van Pluijm amesema anawaheshimu sana wapinzani wake timu ya Gor Mahia lakini hawaogopi na anamatumaini makubwa ya kufanya vizuri kwenye michuano hiyo.
“Nimekuwa Afrika tangu mwaka 1996 hivyo ninauzoefu na soka la timu za hapa kwa muda mrefu, tumefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya kuikabili kila timu kwenye michuano hii. Kitu kikubwa ni kwamba, mimi huwa sidharau mpinzani wangu kwasababu kwenye soka lolote linaweza kutokea na hakuna mtu anayejua matokeo”, amesema Pluijm.
Kocha mkuu wa Gor Mahia Frank Nuttal akizungumza na waandishi wa habari
Kocha mkuu wa Gor Mahia Frank Nuttal akizungumza na waandishi wa habari
Kwa upande wake kocha mkuu wa Gor Mahia Mcotish  Frank Nuttal amesema yeye hana uzoefu mkubwa kwenye soka la Afrika ukilinganisha na mpinzani wake (Van Pluijm) lakini akasisitiza kuwa vijana wake wako vizuri kuikabili Yanga kesho kwenye uwanja wa Taifa.
“Yanga ni timu kubwa japo sijawahi kuiona ikicheza lakini naamini ni timu yenye ushindani na mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini mwisho wa mchezo tutajua matokeo”, amesema kocha huyo.
Van Pluijm 2Mchezo mwingine wa kundi A utachezwa kwenye uwanja wa Karume ukizikutanisha KMKM dhidi ya Telecom kutoka Djibouti


Screen-Shot-2015-07-17-at-9.14.56-AM              STORI NYINGINE MBAYA KWA KLABU YA MANCHESTER UNTED MADRID WAGOMA KUMUUZA RAMOSI
Kocha mpya wa Real Madrid, Rafa Benitez jana katika mkutano na waandishi wa habari nchini Australia ameulizwa hatima ya beki wake, Sergio Ramos.
Ramos, 29, amekuwa gumzo majira haya ya kiangazi na inaelezwa kwamba Mhispania huyo anataka kuondoka Real kutokana na kukosekana kwa maelewano baina yake na uongozi wa klabu.
Manchester United wamekuwa wakihusishwa kumsajili Ramos, wakati huo huo nao Real Madrid wakiomba kumsajili golikipa wa Old Trafford, David De Gea.
Je, Benitez amaejibu nini?
Kocha huyo wa zamani wa Liverpool na Chelsea amethibitisha kwamba Man United wanamuwinda Sergio Ramos, lakini akawaambia watu wengi waliohudhuria mkutano huo kuwa mlinzi huyo kisiki hauzwi.
‘Kuna mengi yanazungumzwa kuhusu hatima ya Ramos. Mimi nashangaa kwasababu mchezaji mwenyewe anajituma kwenye mazoezi na anafanya kila kitu timu inataka na mimi pia ninachotaka”.
Tayari Rais amezungumzia hilo kuwa Ramos atabakia klabuni.
Nimezungumza naye kwa kirefu kuhusu hatima yake. Naona Segio ni mtu muhimu kwenye timu. Ni mshindi na ndio maana tunamhitaji kwenye timu”. Amesema Benitez.
Wakati huo, mpenzi wa Ramos, Pilar Rubio ambaye ni mjamzito amewaambia waandishi wa habari wiki hii kwamba atakwenda Manchester kama mpenzi wake akiuzwa na akathibitisha kwamba wameanza kujifunza kuongea kiingereza.
 
RONALDO AANZA RASMI MAZOEZI KUJIANDAA NA MSIMU MPYA LIGI KUU HISPANIA
 12 
 
Cristiano Ronaldo  kiasili ni mtu wa ushindani, anapenda kushinda bila kujali ni tukio gani anashindania.
 
Mwanasoka huyo anayeshikilia tuzo ya Ballon D’Or ameshangilia ushindi mdogo tu katika mazoezi na wenzake kama anavyofanya kwenye mechi za ligi ya mabingwa.
 
Cheki hapa alivyofanya baada ya kufanikiwa kuingiza mpira na kumfumua Illaramendi Wakati wa mazoezi ya  cone drill.
 
Ameshangilia staili yake ya  ‘SIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII!’ baada ya kupata pointi kama alivyofanya  baada ya kushinda Ballon D’Or mwezi Januari mwaka huu,
 
Maskini Illara.
 

c


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni